The House of Favourite Newspapers

Umoja wa Afrika Kujiondoa Katika Mahakama ya ICC

Umoja wa Afrika umeunga mkono mpango wa kujiondoa kwa pamoja katika mahakama ya ICC ambayo mataifa mengi ya Afrika yanahisi inawalenga viongozi wa Bara la Afrika pekee.

Uamuzi huo uliochukuliwa katika kikao cha faragha haujahalalisha hatua hiyo.

Viongozi wa Afrika wanasema kuwa mahakama hiyo ilikosea kumlenga rais wa Sudan Omar El Bashir kwa mauaji ya Darfur na Uhuru Kenyatta wa Kenya kwa kuchochea ghasia za baada ya uchaguzi.

Mpango huo unapendekeza kwamba mataifa ya Afrika yanafaa kuimarisha mahakama zake na kupanua uwezo wa mahakama ya Afrika kuhusu haki na haki za binaadamu.

CHANZO: BBC SWAHILI

Save

Shinda Nyumba Awamu ya Pili Yatikisa Jiji la Dar es Salaam

Save

Comments are closed.