Mahakama ya Hakimu Makazi Mbeya leo inatarajia kutoa hukumu ya kesi ya kumkashifu Rais Dkt. Jonh Magufuli inayowakabili Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi na Katibu wa CHADEMA Nyanda ya Juu Kusini, Emmanuel Masonga.
Watuhumiwa ambao ni Sugu na Masonga tayari wameshafika mahakamani hapo huku ulinzi ukiwa umeimarishwa katika eneo la Mahakama.
Wengine ambao tayari wameshafika mahakamani hapo ni makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Profesa Abdallah Safari, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Bara, John Mnyika, mke wa Sugu na wengine.
Tayari Sugu na Masonga wameingia ndani ya mahakam hiyo na kesi hukumu yao imeshaanza kusikilizwa.
Comments are closed.