The House of Favourite Newspapers

Usiku wa Raha za Pwani Waja, Khadija Yusuf, Kivurande, Msagasumu, Misambano Ndani

0
Mashabiki wa Kundi la Kivurande linalotarajiwa kufanya balaa Agosti 30 mwaka huu walivyokuwa wakijiachia kwenye uzinduzi wa kundi hilo uliofanyika mwezi ulipita ndani ya Ukumbi wa Mbizo Garden uliopo Magomeni Dar.

 

NGOMA inogile: Usiku wa Raha za Pwani waja, hivyo ndivyo unavyoweza kusema kufuatia burudani ya aina yake iliyoandaliwa na Kampuni ya Mbizo Entertainment ndani ya ukumbi wa burudani wa Mbizo Garden uliopo Magomeni Dar ambayo itafanyika Agosti 30 mwaka huu.

Akizungumza na paparazi wetu muandaa wa burudani hiyo, Mkurugenzi wa Mbizo Entertainment, Juma Mbizo amesema usiku huo si wa kulala na kusubiri kuhadithiwa usije sumbua watu.

Abdul Misambano aliwapagawisha mashabiki waliofika kwenye uzinduzi wa kundi la Kivurande naye atakuwepo kufanya yake hiyo Agosti 30 mwaka huu kwenye usiku huo wa raha.

 

 

Mbizo amesema katika usiku huo kutakuwa na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali yakiwemo makundi ya taarab ya Jahazi, East African Melody, Zanzibar Stars. Bendi ya Maquis International chini ya Bobo Sukari nayo itafanya yake ukumbini hapo na kunogesha usiku huo.

 

Mbizo aliwataja wasanii wengine kwenye usiku huo kuwa ni pamoja na Abdul Misambano, Msagasumu bila kusahau mdatishaji wa mjini mwenye vigoma vyake vya kibao kata almaarufu Kivurande ambaye kundi lake lilizinduliwa rasmi hivi karibuni.

Mfalme Mzee Yusuf na kundi lake la Jahazi Modern Taarab naye amepania kukiwasha na kudhihirisha ufalme wake siku hiyo.

 

Watoa burudani hao kila mmoja na kila kundi limeahidi kumfunika mwenzake na kuugeuza usiku huo kutoka usiku wa raha kuwa usiku wa kufunikana na kuacha gumzo.

Leave A Reply