The House of Favourite Newspapers

Watu zaidi ya 800,000 wameitazama “Utanipenda ya Diamond” ndani ya wiki!

DiamondVideo mpya ya staa wa Bongo Fleva, Diamond Platinumz imetazamwa na watu  zaidi ya laki nane na tisini kwa muda wa wiki moja tangu itoke Desemba 11, mwaka huu.

Mkali huyo wa Bongo Fleva anatarajia kuangusha bonge moja la shoo ndani ya Ukumbi wa Dar Live, Mbagala-Zakhem, jijini Dar siku ya Krismasi, keshokutwa.

DIAMOND (3) Staa wa Bongo Fleva, Diamond Platinumz.

Akizungumzia maandalizi ya shoo hiyo, Diamond alisema itakuwa ya tofauti. Kila atakayelipia fedha yake ( kawaida shilingi 15,000 na V.I.P shilingi 30,000) hatojutia.

“Tukutane pale Dar Live, tuimbe na kucheza nyimbo zote za Diamond kuanzia Kamwambie, Lala Salama, Moyo Wangu, Mbagala, Nimpende Nani, Nitarejea, Ukimuona, Nataka Kulewa, Kesho, Nasema Nao, Mawazo, Number One, Nana, Nitampata Wapi, Kizaizai, MdogoMdogo, BamBam na Utanipenda ambao ndiyo habari ya mjini kwa sasa,” alisema Diamond.

 

Comments are closed.