UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) umeanzisha mpango wa kuwasaidia wanachuo wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu jinsi ya kujaza fomu na kuomba mkopo kupitia Bodi ya Mikopo ya kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB).
Akizungumza na mwandishi wetu, ofisa wa UVCCM, Mwanaidi Kipingu, amesema msaada huo wanautoa bila kuangalia itikadi za kisiasa wala zozote zile.
Aidha amewataka wanafunzi wote wanaohitaji kuomba mikopo hiyo wajitokeze mapema katika ofisi za UVCCM zilizopo makutano ya Barabara ya Morogoro na Lumumba Dar es Salaam.
Mwanafunzi Mwamvua Hussein ambaye alimaliza diploma na kufika ofisi hizo kwa ajili ya mkopo wa kumwezesha kusoma digrii akishukuru baada ya kukamilisha mchakato huo
HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS /GPL
Comments are closed.