The House of Favourite Newspapers

UWT Taifa Yawahasa Vijana Kuwa Wazalendo

Jumuiya ya umoja wa wanawake Taifa (UWT) imewahasa vijana na  wanafunzi wa shule mbalimbali hapa nchini kuwa na uzalendo ili kutumikia nchi yao hususani wanaomaliza  kidato cha sita na kupata nafasi ya kwenda katika mafunzo ya jeshi la kujenga Taifa .

Hayo yamesemwa na Mjumbe wa Baraza kuu la UWT  Taifa  Lucy Edward Mwakyembe kwa niaba ya Mwenyekiti wa UWT Taifa Mary Chatada baada ya kutembelea na kukagua ujenzi wa vyumba  5 vya madarasa katika shule ya sekondari Chabalisa iliyopo kata ya Nyabiyonza wilaya ya Karagwe vilivyoghramu milioni 100.

Akizungumza na wanafunzi pamoja  na wananchi  katika shule hiyo Mwakyembe amesema kuwa baadhi ya vijana wamekuwa na tabia ya kukataa kwenda jeshini kwa kusingizia kuwa ni mateso ambapo usababisha  kukosa uzalendo na kujiingiza katika matendo yasikuwa na maadili ya Kitanzania ikiwemo Ushoga na Usagaji.

“Wazazi tushirikiane  kuwaelimisha watoto kutojihusisha kabisa na utamaduni wa nje ambao si maadili ya Kitanzania kama vitendo vya Ushoga na Usagaji,watoto wetu wakiaribika awatapata wanawake au wanaume wa kuoa na kuolewa kwahiyo ni muhimu wazazi tubebe swala hili kwa umuhimu mkubwa” alisema Mwakyembe

Aidha amewahasa wanafunzi wa shule hiyo kujikita katika masomo na kutokubali kujiingiza katika matendo maovu na kutambua elimu ndo nguzo muhimu katika maisha huku akiwataka wazazi na walezi kupinga vikali ukatili wa kijinsia ambao umeshamili katika baadhi ya maneno hapa nchini.

Kwa upande wake  Katibu Msaidizi Mkuu Utawala UWT Taifa Ndg Jenifer Chingulile amesema wapo baadhi ya wazazi ambao wanawakataza watoto kwenda kujiunga na jeshi la kujenga Taifa (JKT) pindi wanapomaliza kidato cha sita wakizani kuwa ni kwenda kupoteza muda jambo ambalo sio sahihi.

“Serikali inayoongozwa na chama cha mapinduzi Ccm haiwezi kupoteza fedha kuwapeleka vijana jeshini pasipo kuwa na faida hivyo ni muhimu vijana hususani waliomaliza kidato cha sita kwenda jeshini kujifunza uzalendo na kujifunza maadili mema ya Kitanzania na kujiepusha na  suala la ushoga na usagaji” Alisema Jenifer.

Hata hivyo wananchi wa kijiji cha Nyabiyonza walipata nafasi ya  kuwasilisha changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo changamoto ya vitambulisho vya NIDA ambapo Mjumbe Baraza kuu la UWT Taifa ameahidi Chama cha mapinduzi CCM kitazitatua changamoto hizo.

Jumuiya ya umoja wa Wanawake Taifa (UWT) ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mary Chatada inaendelea na ziara ya kikazi mkoani kagera ambayo ilianza mapema wiki hii kwa kukagua miradi  ya maendeleo pamoja na kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali za Wananchi.

MAMA WARDA AKUTANA USO KWA USO NA MWALIMU WEMA, VILIO VIPO PALEPALE | MAPITO