‘SIKU YA WAPENDANAO’ ILIVYODAMSHI NDANI YA DAR LIVE
USIKU wa kuamkia jana ulimwengu ulisherehekea Siku ya Wapendanao ambapo katika Jiji la Dar es Salaam moja ya sherehe kubwa za kuadhimisha siku hiyo nchini, ilifanyika Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live ulioko kitongoji cha Mbagala-Zakhem jijini Dar es Salaam.
Uwanja huo ulijaa kila aina ya nuru za watu, nguo na vitu, zikiwemo zawadi mbalimbali kuadhimisha siku hiyo inayochochea upendo kwa watu wanaopendana.
Wakati wote huo wapendanao hao walikuwa wakichombezwa na nyimbo za kimahaba kutoka kwa mkali wa nyimbo za kubembeleza, Beka Ibrozama, aliyekuwa akibadilishana jukwaa na mkali wa nyimbo za kimahaba zenye mahadhi ya kimwambao.
Wengine walionogesha mambo ni kundi la YAH TMK Modern Taarab na Khanifa Maulid ‘Jike la Chui’.
PICHA: RICHARD BUKOS / GPL
Comments are closed.