The House of Favourite Newspapers

Vera, Bwana’ke Wachafua Mitandao

Vera Sidika na Otile Brown

SAHAU kuhusu ule ujauzito wake feki ‘ulio-trendi’ juzikati, muuza nyago kwenye video nchini Kenya, Vera Sidika amechafua mitandao baada ya kuanika picha tata akiwa na mtu anayedaiwa ni mpenzi wake ambaye ni mwanamuziki nchini humo, Otile Brown.

 

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Vera ndiye aliyeanza kutupia picha hizo ambazo zinamuonesha akiwa ameshikwa na Otile kama mtu anayetaka kunyongwa huku akiwa kifua wazi kitandani.

 

Muda mchache baada ya Vera kuposti hivyo, Otile naye akaamua kujibu kwa kuachia picha akimchezea eneo la shingoni kwa mdomo, jambo lililofanya picha hizo kuenea kila kona ya mitandao hasa ya nchini Kenya.

NAIROBI, Kenya

 

Comments are closed.