The House of Favourite Newspapers

VIDEO: ALIKIBA ATOA TAMKO RASMI MBELE YA WAANDISHI DAR

MSANII wa Bongo Fleva, AliKiba leo Novemba 8, 2019 amezungumza na waandishi wa habari katika hoteli ya Ramada Posta jijini Dar es Salaam amesema hana ugomvi na Diamond Platnumz ila hawezi kushiriki kwenye tamasha lake kwa sababu na yeye anatafuta mafanikio.

Kiba amelazimika kutoa ufafanuzi kuhusu suala hilo mara ya pili, wiki iliyopita Diamond alisema uongozi wa lebo ya WCB unafanya mazungumzo na Kiba ili akatumbuize kwenye tamasha la Wasafi linalofanyika kesho kwenye viwanja vya Posta Kijitonyama Jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Comments are closed.