The House of Favourite Newspapers
gunners X

Video: JPM Akabidhi Tausi Marais Wastaafu Dodoma

0

 

Rais John Magufuli akikabidhi hati ya makabidhiano ya zawadi ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Mama Maria Nyerere, mjane wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere,  kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake.  Hafla hiyo fupi ilifanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma.

RAIS John Magufuli leo Mei 30, 2020,  amewakabidhi ndege 25 aina ya tausi kila mmoja, marais wa awamu zilizopita kwa ajili ya kupamba bustani za makazi yao.

…Akimkabidhi   Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi .

Marais hao ni Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete na marehemu Mwalimu Julius Nyerere ambapo zawadi hiyo ilipokelewa na mkewe (mjane), Mama Maria Nyerere.

Tukio hilo limefanyika makao makuu ya nchi jijini Dodoma wakati wa sherehe ya kuzindua ujenzi wa ofisi za ikulu ambapo alisema  amefanya juhudi kubwa katika kuwatunza tausi 403 aliowakuta ambapo hadi sasa kuna tausi 2,260 katika bustani za Ikulu ya Dodoma na Dar es Salaam.

Magufuli alisema aliongeza idadi ya ndege hao wenye kuvutia kwa kununua mashine ya kusaidia kutotolea mayai ya ndege yao, jambo lililosababisha kuongezeka kwake, tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma.

Rais mstaafu, Jakaya Kikwete, alimshukuru Magufuli kwa kuwatunuku zawadi hiyo.

…Akimkabidhi Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa.
…Akimkabidhi  Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete.

Tazama video ya chini kwa habari zaidi.

Leave A Reply