The House of Favourite Newspapers

VIDEO: MFUNGWA Amshtaki ASKARI Kwa MAGUFULI – “ATATUUA ONDOKA NAE”

Miongoni mwa wafungwa wa Gereza la Butimba jijini Mwanza ambaye alikuwa wa kwanza kuzungumza ni Kalikenya Nyamboge aliyesema:

“Mheshimiwa rais kuna ofisa usalama yuko huku ndani anawapa wafungwa simu halafu zikikamatwa tunanyan’ganywa vitu vyetu lakini hadi leo hajafanywa kitu chochote.

“Mheshimiwa rais huyu ofisa akupe mihuri na hizo simu uondoke nazo utajua mwenyewe utaenda kufanyia nini na ikibidi ondoka naye kwani ukifanya hivyo utakiwa umetusaidia sana na ukimuacha atanidhuru.

“Sasa hivi Jenerali Kamishna ametuletea daktari msomi na alivyofika vifo ndiyo vimepungua maana walikuwa wakikuchoma sindano wanakuua.”

Comments are closed.