MWILI wa dada wa Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Global Group, Eric Shigongo, marehemu Vaileth James Bukumbi, umewasili leo Alhamisi, Juni 20, 2019, nyumbani kwao katika Kijiji cha Bupandwamhela, Buchosa – Sengerema mkoani Mwanza kwa ajili ya maziko.
Msafara wa uliyokuwa na mwili huo kutokea maeneo ya Nyamhongolo, nje kidogo ya jiji la Mwanza alikokuwa akiishi marehemu, umepokelewa na umati mkubwa wa waombolezaji, ndugu, jamaa na marafiki waliokuwa wakisubiri kuupokea mwili wa ndugu yao mpendwa ambaye aliaga dunia usiku wa kuamkia juzi Juni 18, 2019 jijini humo.
Vilio, simanzi na majonzi vimetawala wakati wa kuupokea mwili huo miongoni mwa waombolezaji wakiwemo watoto wake, dada zake, kaka zake na ndugu wote wa familia ya marehemu Mzee James Bukumbi.
Mwili wa marehemu Vaileth unatarajiwa kuagwa na kuzikwa kesho nyumbani kwao Bupandwamhela ambako wazazi wake, Mzee James Bukumbi na Bi Asteria Kapera aliyeaga dunia Julai mwaka jana, wote wamezikwa hapo.
PICHA NA DENIS MTIMA | GPL
Comments are closed.