The House of Favourite Newspapers

Vipigo vya Simba vyamchosha Twite Yanga

0

MBUYUTWITESALAMAJAMANIPIXNO5KIRAKA wa Yanga, Mbuyu Twite amesema amechoshwa kufungwa na Simba kila mara, hivyo leo vyovyote itakavyokuwa ni lazima timu yake ishinde.

Simba na Yanga zinacheza mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa huku Wanajangwani wakiwa na kumbukumbu ya kufungwa bao 1-0 katika mchezo wa mwisho katika ligi zilipokutana Machi, mwaka huu.

Akizungumza na Championi Jumamosi kutoka Pemba ilipokuwa kambi yao, Twite alisema yeye pamoja na wenzake wamechoshwa na vipigo kutoka Simba na sasa wameamua kuwageuzia kibao.

Mara ya mwisho kwa Yanga kuifunga Simba ilikuwa Mei 18, 2013 ilipoibuka na ushindi wa mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Taifa chini ya Kocha Ernie Brandts raia wa Uholanzi.

“Msimu huu lazima tuifunge Simba iwe isiwe kwani tumechoka na uteja, hivyo tumejipanga kuhakikisha tunashinda, naamini kambi yetu ya Pemba itatusaidia.

“Kikosi chetu kizuri na tunahitaji kushinda mechi zetu zote zilizo mbele ili kuweza kutetea ubingwa wetu,” alisema Twite anayemudu kucheza kiungo, pia beki wa kulia hata katikati.

JIUNGE NA VODACOM MICHEZO KIGANJANI.

CHAMPIONIMBUYUTWITESALAMAJAMANIPIXNO5

Leave A Reply