The House of Favourite Newspapers

VODACOM YAKABIDHI ZAWADI ZA WASHINDI WA VPL 2017/18

Meneja wa Yanga, Hafidhi Saleh, akiwa ameshika hundi ya klabu yake ya milioni thelathini na nane, laki tatu themanini na tisa, mia tisa na ishirini,  baada ya kukabidhiwa na mdhamini wa Ligi Kuu Bara usiku wa kuamkia leo Mlimani City jijini Dar.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akiwa na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Wallace Karia (kushoto) na Meneja Mauzo wa Vodacom.
Msemaji wa klabu ya Azam, Jaffari Idd Maganga (kulia) akiwa na hundi ya klabu iliyoshika nafasi ya pili katika Ligi Kuu ya Vodacom.
Mwakyembe (katikati) akikabidhi hundi ya sh. milioni 96 kwa Kaimu Rais wa Simba, Salim Abdallah ‘Try Again’ (kushoto).  Simba ilipata tuzo hiyo kwa kutwaa ubingwa wa Vodacom kwa msimu wa 2017/18.
Mdau wa klabu ya Simba, Abdallah Kibaden (kulia) akiwa na wadau wa hafla hiyo alipopokea hundi ya milioni tatu ya Mfungaji Bora wa msimu wa 2017/18 iliyotolewa kwa  Emmanuel Okwi.

Usiku wa June 23,  2018 ulishuhudia utoaji wa Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2017/18 kwa washiriki na wadau waliofanya vizuri katika ligi hiyo ikiwa ni pamoja na makocha, wachezaji na kadhalika.

Tuzo ya Mfungaji Bora ilienda kwa Emmanuel Okwi wa Simba mwenye mabao 17 ambaye alituzwa Sh milioni tatu. Kwa timu zilizoshika nafasi mbalimbali,  nafasi ya nne ilichukuliwa na Prisons ya Mbeya ambayo ilipata Sh mil. 27,  Yanga ya tatu ilipata mil. 34, Azam ya pili ilipata mil. 48 na mabingwa Simba mil. 96.

PICHA: RICHARD BUKOS | GPL

Comments are closed.