The House of Favourite Newspapers

Wachawi wamtaka Wastara akiwa bado tumboni

0
Wastara Juma.

 

ILIPOISHIA…

MPENZI msomaji baada ya kuwa nami mwan­zomwisho katika simulizi ya maisha ya Asha Baraka, mmiliki wa Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’, nachukua wasaa mwingine kukukari­bisha katika simuli­zi ya maisha ya mui­gizaji mwenye jina kubwa na heshima katika Tasnia ya Filamu Tanzania, Wastara Juma.

Wastara ni mui­gizaji aliyeanza kujipatia umaarufu zaidi akiwa chini ya kampuni ya kuan­daa filamu iitwayo Wajey ambayo alikuwa akiimiliki pamoja na marehe­mu mumewe Juma Kilowoko ‘Sajuki’. Ameigiza muvi nyingi ikiwemo Mboni ya Jicho Langu, Vita, Detec­tive na nyingine za hivi karibuni. Hapa anafunguka mwan­zo mwisho historia ya maisha yake.

 

…SASA ENDELEA

“NIMEZALIWA mwaka 1983 huko Mvomelo mkoani Morogoro. Mimi ni mtoto wa tano kati ya saba wa mama yangu Hamida na baba yangu Juma Issa. Kabila la mama yangu ni Al Liwail na baba yangu ni Al Rawahi ambao asi­li yao ni huko Muscat, Oman.

“Hata hivyo ni­mechanganyikana na Wa­hindi na Wanyamwezi, kwa upande wa bibi aliyem­zaa mama yangu, lakini bibi mzaa baba ni Mma­sai. Wakati huo tunaza­liwa, baba yangu alikuwa ni dereva na mama alikuwa akifanya biashara ya ku­uza chakula,” anaanza kusimulia Wastara.

 

Wastara anaendelea kuwa katika maisha yake amepitia misukosuko mingi sana na yenye kuu­miza. Anasema misuko­suko hiyo ilianza hata kabla hajazaliwa maana aliwahi kusimuliwa na mama yake kuwa wakati akiwa na ujauzito wake wenye muda wa miezi sita, siku moja kuna sehemu alipita majira ya jioni.

Anasema sehemu hiyo ilikuwa ni ya vichaka na hakukuwa na watu wana­pita mara kwa mara. Mama yake akiendelea kutembea Wastara anasimulia alihisi kuna watu walikuwa wan­amfuata nyuma lakini al­ipokuwa akigeuka hakuwa anawaona.

 

“Sasa mama yangu ni mtu ambaye ni kama alikuwa na maono hivi. Japo alikuwa hawaoni watu hao lakini kwa namna mwili ul­ivyokuwa unamsisimka ali­fahamu wapo na walikuwa wakimfuatilia. Akaamua kuongea na kuwaambia wajitokeze ili wazungumze na kusema wanataka nini.

“Kweli baada ya kusema hivyo walijitoke­za watu ambao anaamini wa­likuwa ni wach­awi. Akawauliza wanataka nini w a k a m w a m ­bia wanamtaka mtoto ambaye alikuwa tumboni mwake maana alikuwa ni mzuri sana.

 

“Mama ali­wakatalia na ku­waambia wata­hangaika sana lakini hawatawe­za kumpata mto­to wake. Baada ya kuwaambia hivyo wale wachawi walipotea na ku­muacha akaon­doka zake. Siku zi­kasonga mbele na hatimaye muda wa mama kujifun­gua ukawadia,” anasimulia Wastara.

Anaendelea kuwa siku chache baada ya kujifungua mama yake aliugua mno kiasi kwamba akawa hawe­zi kumnyonyesha kabisa kichanga wake. Wastara akawa analelewa na mfan­yakazi wa ndani ‘housegirl’. Baada ya kuugua muda mrefu mama yake alipele­kwa kwa mashehe na ku­fanyiwa dua ambapo baa­daye akapona na kubeba ujauzito mwingine.

 

Lakini mtoto aliyejifun­gua alipatwa na matatizo makubwa ambayo alitak­iwa kuyapata Wastara. Akiwa tu na miezi sita al­ianza kuugua ambapo hadi miaka miwili alikuwa hawezi kuzungumza na hali ikaendelea hivyo mpaka al­ipokuwa na miaka saba.

Wastara anaendelea kusimulia kuwa kwa up­ande wake ‘series’ ya misu­kosuko ilianza kutiririka, ukiachana na tukio la ku­takiwa na wachawi akiwa bado mtoto mdogo sana am­baye hajafika hata umri wa kuanza shule.

 

Anasema wakati huo aliwahi kuu­gua ugonjwa wa Kifaduro ambao ulimsumbua mno. Anasema alikuwa kwenye hali mbaya kiasi kwamba alikuwa anaji­saidia haja kubwa muda wote na po­pote pale. Wastara anafunguka wazazi wake walihangaika naye kwenye hos­pitali mbalimbali Morogoro lakini hakuweza kufani­kiwa kupona. Aka­pelekwa Tumbi na hatimaye akapona alipofikishwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

“Siku zikaendelea ku­songa mbele na baada ya kurudishwa nyumbani maisha yakaendelea. Sasa siku moja mimi na kaka yangu ambaye ninamfua­ta, tulikuwa tunaendesha matairi njiani. Ulikuwa ni mchezo wa kawaida tu am­bao watoto enzi hizo wali­pendelea kufanya.

 

“Tukiendelea kuende­sha mara kuna pikipiki ili­kuja nyuma yetu. Tukawa tunakimbia kuikwepa la­kini ikawa inatufuata tu. Tukienda upande wa kulia inatufuata, upande wa kushoto na bado inatu­fuata. Sasa mimi nikaamua kusimama katikati ya bara­bara. Ndipo ikaja na kuni­pitia PUUUU! Nikadondoka pembeni. Nilikuja kurejewa fahamu nikiwa katika Hos­pitali ya Bwagala iliyopo Tu­riani, Morogoro na nilikuwa nimevunjika miguu miwili.

 

“Hapo nilipewa tiba la­kini sikuweza kufanikiwa kupona nikarudishwa ny­umbani. Mwaka mzima ukakatika nikisota chini, nikawa mlemavu, kila kitu nikawa nasaidiwa hapo­hapo!”

Je, nini kitaendelea? Kipi kilitokea mpaka aka­pona tena miguu? Ni ma­tukio gani ambayo mwa­nadada huyu amekutana nayo kwenye maisha yake? Usikose wiki ijayo.

Mwandishi: Boniphace Ngumije

Msimuliaji: Watara Juma

Makala Kutoka Gazeti la Championi Jumatatu | Staa anayefunguka

 

LIVE: Ibada ya Kuaga Mwili wa Mke wa Mwakyembe, KKKT Kunduchi-Dar

Leave A Reply