The House of Favourite Newspapers

Wachina Wamchizisha Costa

0

diego-costa

Makala: Gazeti la Championi, Toleo la Jumatatu, Januari 16, 2017

LONDON, England

DIEGO Costa kazingua tena. Kibaya zaidi katibua wakati Chelsea ikiwa im­ekoleza vita ya kuwania ubingwa wa Premier na yeye ndiye akiwa mchezaji anayetegemewa zaidi na klabu hiyo katika kupachi­ka mabao.

Wiki iliyopita, straika huyo ambaye hadi juzi alikuwa kinara wa mabao kwenye Premier, alitoleana maneno makali na kocha wake Antonio Conte, kiasi cha kulazimika kutupwa nje ka­tika kikosi kilichoivaa Leicester City juzi usiku.

Costa hakusafiri na kikosi cha Chelsea kilichokwenda jijini Leicester kuvaana na mabingwa hao watetezi kutokana na kutokukubaliana na ma­bosi wake kuhusu suala la majeraha yake.

costa_3082271bCosta, 28, anaamini ana tatizo la mgongo wa chini ambalo linatokana na mfululizo wa matatizo ya nyama za paja ambayo yamekuwa yakimsum­bua kwa muda mrefu.

Alitaka wiki iliyopita apumzike lakini Chelsea ilitarajia afanye mazoezi katika programu ya ma­zoezi magumu ya Conte, hata hivyo hakufanya mazoezi kwa siku tatu.

Kitendo hicho kilisababi­sha azozane kinoma na ko­cha wa viungo wa Chelsea na baadaye mzozo huo ukawa dhidi yake na Conte.

Tukio hilo limetokea siku chache baada ya Costa kupokea ofa nono kutoka China, huku ikiripotiwa kuwa kuna klabu moja imemwam­bia Mhispania huyo kwamba ipo tayari kum­lipa kiasi cha pauni milioni 30 (karibu bilioni 80) kwa mwaka aondoke Stamford Bridge.

Hiyo itamaanisha kwamba atakuwa ak­ipokea mshahara wa pauni 576,923 (Sh bil­ioni 1.5) kwa wiki, ambao hauko mbali na ule wa mwanasoka anayelipwa vizuri zaidi duniani, Carlos Tevez ambaye anapokea ki­tita cha pauni 615,000 (Sh bilioni 1.63) kwa wiki ambacho kinamfanya afanye chochote anachotaka kinachohitaji fedha katika dunia hii.

Inaaminika tayari wawak­ilishi wa Costa wapo China. Oscar na John Mikel Obi tayari walishaitosa Chelsea na kwenda kwenye dunia ya pesa (China).

Katika mzozo kati yake na Conte, ko­cha huyo Muitaliano ambaye naye ni mtata kwelikweli, inadaiwa alisikika akimbwatukia Cos­ta akimwambia: “Nenda China tu.”

Klabu ya Tianjin Quanjian, ambayo imemsajili kiungo Mbelgiji, Axel Witsel, ipo sokoni ikisaka straika na imekuwa ikihusishwa na Costa kwa dau la pauni milioni 80.

Chelsea walikuwa na matumaini ya kukubal­iana mkataba na Costa baada ya straika huyo awali kutamka kuwa ana furaha sana kuendelea kuichezea timu hiyo, la­kini ishu hii iliyotokea wiki iliyopita imeibua utata.

C h e l s e a inatarajia su­ala hili liiishe haraka lakini limemuacha Conte akiwa na pasua kichwa kwa kuwa anata­ka timu yake irejee kwenye hali ya kushinda mfululizo.

Hadi kabla ya mechi za juzi, Costa alikuwa akiongoza kwa mabao kwenye Premier akiwa na mabao 14 na ilionekana kama nidhamu yake imepan­da sana msimu huu, baada ya wakati fulani kucheza mechi 11 bila kuonyeshwa kadi, kitu ambacho kilikuwa nadra sana kwake katika misimu iliyopita.

Wawili hao walionekana kuwa na uhusiano mzuri, licha ya Costa kumbwatukia Conte katika ushindi dhidi ya Leices­ter mwaka jana, akionyesha ishara kwamba anataka ku­tolewa uwanjani ili kuepuka kupewa kadi na kuikosa mechi dhidi ya Manchester United kwa kuwa timu yake ilikuwa tayari na uhakika wa kushinda. Costa alionywa asirudie tabia hiyo.

Wiki moja tu iliyopita katika mchezo dhidi ya Tottenham ambao Chelsea iliambulia ki­pigo, Costa alikuwa katika sekeseke lingine baada ya kum­bwatukia mchezaji mwenzake Pedro kwamba hakukimbia kwa mahesabu baa­da ya kupoteza nafasi. Conte alipuuza ishu hiyo akidai ni hali ya kawaida uwanjani.

Kuna matukio mengine mengi ya Costa kulianzisha mazoezini lakini yamekuwa yakitulizwa na kuzimwa kimyakimya.

Hata hivyo, inaonekana ni afadhali sana msimu huu kwa Costa ukilinganisha na msimu uliopita ambao alifikia hatua ya kumtupia nguo (bips) kocha wake Jose Mourinho kisa kum­toa nje, pia kugombana maz­oezini na mchezaji mwenzake Oscar ambaye hivi sasa amek­wenda China.

Suala la Costa linaweza kumshinikiza Conte atafute straika katika dirisha hili la Jan­uari. Anavutiwa kumsajili Fern­ando Llorente kutoka Swansea na kumbakiza Michy Batsh­uayi ambaye anatakiwa kwa mkopo West Ham, Marseille, Paris St-Germain na Lille.

Lakini swali la wengi ni je, Chelsea itaweza kuendelea vyema katika mbio za ub­ingwa kama suala hili hali­taisha hara­ka?

Leave A Reply