The House of Favourite Newspapers

Wafanyakazi Exim Walivyoshiriki Maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja

Mkuu wa Kitengo cha Hazina na Masoko ya Dunia wa benki ya Exim Tanzania, Nelson Kishanda akizungumza na wafanyakazi wa benki hiyo katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja 2024 katika tawi la benki hiyo la Samora Avenue. Kushoto kwake ni Frank Matoro, Meneja Mkuu wa Huduma za Wateja.

Wafanyakazi wa Benki ya Exim Tanzania wamefanya matembezi ya amani wakati wa kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja 2024 ambapo wametembea kutoka Makao Makuu ya benki hiyo, Exim Tower mpaka tawi lake la Samora Avenue jijini Dar es Salaam mnamo Oktoba 5, 2024.