The House of Favourite Newspapers

Wagosi wa Kaya Waicharaza Yanga Mkwakwani

0

VINARA wa ligi kuu bara Yanga leo Machi 4, wameshindwa kufurukuta katika dimba la mkwakwani jijini Tanga, baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya wenyeji wa mchezo huo Coastal Union.

 

Ikishuka dimbani mara ya 22, Yanga ambayo ilikuwa inashikilia rekodi ya kutofungwa msimu, imeshindwa kuendeleza rekodi hiyo  na kujiweka kwenye mazingira magumu ya kuongoza ligi hiyo.

 

Yanga ilianza mechi kwa kasi ikicheza soka la kushambulia na kufanikiwa kupata  penati, ambayo hata hivyo mpigaji Tuisila Kisinda alikosa baada ya kipa kudaka mkwaju wake.

 

Iliwachukua dakika moja Coastal Union kufunga  bao la kuongoza kupitia kwa mchezaji Erick Msagati dakika ya 10, baada ya mlinda mlango wa Yanga Farouk Shikalo kushindwa mpira wa  krosi.

Alikuwa Kisinda aliyewarudisha mchezoni wananchi, baada ya kuisawazishia Yanga  dakika ya 37’ na kwenda mapumnziko  matokeo yakiwa ni 1-1.

 

Muuaji wa Yanga alikuwa Mudathir Said aliyepachika bao safi dakika ya 84’ baada ya ngonga nzuri kutoka kwa Wagosi wa kaya na kuihakikishia timu alama tatu.

 

Yanga bado inaongoza ligi ikiwa na alama 49 baada ya kucheza michezo 22, wakifuatia na watani zao Simba wenye alama 45 wakiwashuka dimbani mara 19, matokeo hayo yanawapa nafasi Simba ya kuongoza ligi endapo atashinda michezo yake viporo.

 

Leave A Reply