The House of Favourite Newspapers

Wahalifu 10 Hatari Zaidi Duniani

Leo nakuletea orodha ya watu kumi hatari zaidi duniani. Wanatafutwa kutokana na matukio mbalimbali ya kihalifu waliyowahi kuyafanya dhidi ya binadamu na mali zao. Baadhi yao tayari wamekamatwa.

10.AYMAN AL-ZAWAHIRI

Mbabe huyu alikuwa kiongozi wa kundi la Egyptian Islamic Jihad lenye makazi yake jijini Cairo, Misri. Ndiye kiongozi wa juu wa sasa wa kundi hatari la kigaidi la Al-Qaeda.

Uhusiano wake wa karibu na gaidi Osama Bin Laden aliyeuawa mwaka 2012 na majeshi ya Marekani ndiyo ulipelekea achaguliwe kuwa kiongozi wa juu wa kundi hili.

Anatajwa kuhusika na ulipuaji majengo ya Pentagon nchini Marekani na mwaka 2012 alitoa waraka wa kutekwa kwa watalii wote wenye uraia wa nchi za Ulaya wanaotembelea nchi za Kiarabu.

-, -:  (FILES) -- A TV grab from the Qatar-based Al-Jazeera news channel dated 17 June 2005 shows Al-Qaeda number two Ayman al-Zawahiri delivering a speech at an undisclosed location with a machine gun next to him. Al-Zawahiri, in a video posted on the Internet 29 September 2006, called US President George W Bush a liar who had "failed in his war against Al-Qaeda", Al-Jazeera television reported. The previous day, Islamist websites on the Internet had said there would be a new video message posted by Zawahiri entitled " Bush, the pope, Darfur and the Crusades."  AFP PHOTO/AL-JAZEERA  -- QATAR OUT & INTERNET OUT --  (Photo credit should read -/AFP/Getty Images)

09.OMID TAHVILI

omid-tahvili

 

Anashika namba tisa kwenye orodha ya watu wanaotafutwa zaidi duniani kwa makosa ya uharifu. Ndiye kiongozi wa kundi hatari la uhalifu la Persian Crime Group lenye makazi yake nchini Canada. Mwaka 2007 alifungwa jela na alifanikiwa kutoroka huku akiacha maswali mengi. Anahusishwa na wizi wa pesa na mtandao wa pesa feki nchini Marekani.

08. FELICIAN KABUGA

Mzee huyu anatajwa kuhusika kwenye mauaji ya kimbari nchini Rwanda ya mwaka 1994 ambapo watu zaidi ya milioni moja waliuawa. Inasemekana amejificha nchini Kenya na juhudi zote za kumkamata zimeshindikana.

felicien kabuga

07. JAMES BULGER

Bulger ni mhalifu sugu nchini Marekani akihusishwa na biashara ya madawa ya kulevya na mauaji ya raia wasio na hatia. Anatajwa kuhusika kwenye matukio ya mauaji zaidi ya 19. Anatafutwa na polisi kwa zaidi ya miaka 30 mpaka sasa na anatajwa kuwa na utajiri unaofikia paundi milioni 18.

whitey-bulger

  1. ALIMZHAN TOKHATHOUNOV

Mafia huyu raia wa Urusi anatajwa kuhusika na biashara ya madawa ya kulevya, utekaji nyara na mauaji ya watu mbalimbali. Anatafutwa na nchi yake na juhudi za kumpata hazijawahi kufanikiwa.

alimzhan-tokhtakhounov

05. JOSEPH KONY

Mpiganaji wa msituni na kiongozi wa kundi la waasi la Lord Resistance Army. Kony raia wa Uganda anayetafutwa kwa zaidi ya miaka 30 sasa, anatajwa kuhusika kwenye mauaji ya raia wengi wasio na hatia, ubakaji na uporaji. Anatafutwa tangu mwaka 1986.

joseph-rao-kony-007

  1. SEMION MOGILEVICH

Anafahamika kwa jina la ‘Mhalifu hatari zaidi duniani’,  anatajwa kuwa kiongozi mkuu wa kundi la mafia la nchini Urusi linalohusika na mauaji mbalimbali na biashara ya madawa ya kulevya.

mogilevich_3175293c

03. DAWOOD IBRAHIM

kiongozi mkuu wa Indian Crime Network kundi hili la wahalifu maarufu kwa jina la D-Company linajihusisha na mauaji ya raia, utekaji, ubakaji na biashara ya madawa ya kulevya kwenye nchi za Pakistan, India na Falme za Kiarabu. Anatajwa kama mmoja wa washirika wa karibu wa kundi la Al-Qaeda.

dawood

  1. MATTEO MESSINA DENARO

Anashikiliwa nchini kwake Italia baada ya kutafutwa kwa miaka zaidi ya ishirini, japo amekamatwa ili kujibu tuhuma zinazo mkabili bado anahitajika nchi mbalimbali duniani kwa kuhusishwa na biashara halamu za madawa ya kulevya na utekaji.

matteoMatteo baada ya kukamatwa.

01. JOAQUÍN GUZMÁN

Huyu ndiye mtu hatari zaidi duniani, maarufu kwa jina la El Chappo, kwasasa anashikiliwa nchini kwake Mexico. Mara zote akikamatwa huwa anatoroka, anatajwa kuwa na kikosi hatari kinachojihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya, huko nchini Marekani wanamtafuta ili wamnyonge.

elchapoEl Chappo baada ya kukamatwa.

Mbali na uhalifu wake pia ni tajiri anayemiliki kiasi kikubwa cha pesa kutokana na biashara hiyo haramu ya madawa ya kulevya. Anahesabika kama mhalifu mwenye nguvu zaidi duniani.

Na Leonard Msigwa/GPL.

 

Comments are closed.