The House of Favourite Newspapers

Wahitimu Chuo Cha Kufundisha Misingi ya Biblia ‘FBTC  Tanzania’Kulinda Maadili

Baadhi ya wahitimu wa mafunzo ya biblia wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi
Baadhi ya wahitimu wa mafunzo ya biblia wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi
Baadhi ya wageni Waalikwa akifuatilia kilichokuwa kikiendelea katika hafla hiyo.
Mchungaji wa Kiongozi wa Kanisa la Pentekoste Assemblies Of God (P.A. G) Mbezi Beach, Mchungaji Kiongozi Thomas Dige akitunukiwa cheti cha kuhitimu mafunzo.
Wahitimu wakiendelea kupokea vyeti vyao.

Mchungaji wa Kiongozi wa Kanisa la Pentekoste Assemblies Of God (P.A. G) Mbezi Beach, Mchungaji Kiongozi Thomas Dige akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mafunzo waliyopata.
Zaidi ya wahitimu 90 Chuo Cha Kufundisha Misingi ya Biblia (FBTC  Tanzania ) wametakiwa kuwa chachu ya maendeleo katika kuhakikisha wanakwenda kusema ukweli, kufichua maovu, kukemea mapenzi ya kijinsia moja  pamoja na kurudisha maadili mema katika jamii.
Akizungumza Jijini Dar es Salaam katika Mahafali ya Pili ya Chuo Cha kufundisha misingi ya Biblia (FBTC  Tanzania ) yaliofanyika katika Kanisa la Pentekoste Assemblies Of God (P.A. G) Mbezi Beach, Katibu Tawala Manispaa ya Kinondoni, Stella Msofe, amesema kuwa viongozi wa dini wanajukumu la kwenda kufundisha maadili ya kitanzania.
Mchungaji wa Kiongozi wa Kanisa la Pentekoste Assemblies Of God (P.A. G) Mbezi Beach, Mchungaji Kiongozi Thomas Dige pamoja na Mkurugenzi wa Mtendaji wa Chuo Cha FBTC  Tanzania, Meshack Mawala, wamesema kuwa kuna umuhimu mkubwa wa kujiunga na masomo katika Chuo hicho, kwani yanakwenda kuleta maisha bora katika jamii, huku wakibainisha kuwa wanaungana na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kudumisha amani.
Hata hivyo baadhi ya wahitimu wamesema kuwa wanakwenda kuyafanyia kazi kwa vitendo kwa lengo la kuisaidia jamii.