Wakazi Chanika wachangamkia droo ya ‘Shinda Nyumba’
Wasomaji wa Gazeti la Championi na Ijumaa wakichangamkia kununua gazeti hizo kutoka kwa muuzaji wa Global (katikati aliye na fulana nyeupe).Wasomaji wa Ijumaa na Championi wa eneo la Chanika-Msumbiji wakiweka kuponi zao kwenye ndoo maalum.
Msomaji wa Gazeti la Championi wa eneo la Kwa-Dadi Chanika akielekezwa na Ofisa Usambazaji wa Global, Jordan Ngowi (kulia) namna ya kujaza kuponi yake.
Ngowi (anayeelekeza katikati) akimwonesha ndoo maalum msomaji wa Gazeti la Championi eneo la stendi ya Chanika mara baada ya kujaza kuponi yake.
Wasomaji wa magazeti ya Championi na Ijumaa wakiwa wamevalia kofia zilizo na nembo ya Shinda Nyumba.
WASOMAJI mbalimbali wa magazeti ya Kampuni ya Global Publishers inayochapisha magazeti ya Uwazi, Amani, Risasi, Ijumaa, Ijumaa Wikienda na Championi,jana walichangamkia droo ya pili ya Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba huko Chanika nje kidogo ya jijini la Dar kwa kujaza kuponi na kushiriki.
Maofisa masoko wa Global, Jordan Ngowi na Yohana Mkanda walitembelea maeneo ya Chanika Msumbiji, Masantula, Magenge, Kwa Dadi na Nzasa-Kwa Mwarabu na kugawa zawadi za kofia zenye nembo ya Shinda Nyumba zilizokuwa zikitolewa baada ya kuwakuta wasomaji wakinunua Gazeti la Ijumaa na Championi.
Akizungumza na wakazi wa maeneo ya Stendi ya daladala ya Chanika, Ofisa Usambazaji wa Global Publishers, Jordan Ngowi, alisema wasomaji wanatakiwa kujitokeza kwa wingi kununua magazeti hayo na kukata kuponi ili kujinyakulia zawadi nyingi kwenye droo ya pili ya Shinda Nyumba inayotarajiwa kufanyika hivi karibuni, sambamba na kujiongezea nafasi ya kushinda zawadi ya nyumba iliyopo eneo la Salasala jijini Dar katika droo ya mwisho.
“Tumekwishatoa zawadi mbalimbali kwa wasomaji wetu kama vile, fulana, kofia, simu za kisasa, runinga na ving’amuzi vya TING katika droo yetu ya kwanza iliyofanyika mwishoni mwa mwezi uliopita.
“Niwasihi wakazi wa Chanika mzidi kununua magazeti yetu ya Global na kujaza kuponi ili muweze kushiriki bahati nasibu yetu. Kitu muhimu cha kuzingatia ni umri usiopungua zaidi ya miaka 18,” alisema Ngowi.
Na Denis Mtima/GPL