The House of Favourite Newspapers
gunners X

Wakurdi waanza oparesheni kukomboa Mji wa Sanjir, Iraq kutoka kwa IS

0

Sinjar  (2)Wanajeshi wa Kikurdi wakijiandaa kukabiliana na mashambulizi dhidi ya IS

sinjarWaumini wa dini ya Yazidi wakikimbia machafuko katika milima ya Sinjar.

This frame grab from Kurdistan 24 video provided to the Associated Press shows smoke believed to be from an airstrike billowing over the northern Iraqi town of Sinjar on Thursday, Nov. 12, 2015. Kurdish Iraqi fighters, backed by the U.S.-led air campaign, launched an assault Thursday aiming to retake the strategic town of Sinjar, which the Islamic State overran last year in an onslaught that caused the flight of tens of thousands of Yazidis and first prompted the U.S. to launch airstrikes against the militants. (Kurdistan 24 via AP)  NO ACCESS KURDISH IRAQMji wa Sinjar baada ya mashambulizi ya anga yaliyofanywa na Wakurdi wakisaidiwa na Marekani.

This frame grab from Kurdistan 24 video provided to the Associated Press shows smoke believed to be from an airstrike billowing over the northern Iraqi town of Sinjar on Thursday, Nov. 12, 2015. Kurdish Iraqi fighters, backed by the U.S.-led air campaign, launched an assault Thursday aiming to retake the strategic town of Sinjar, which the Islamic State overran last year in an onslaught that caused the flight of tens of thousands of Yazidis and first prompted the U.S. to launch airstrikes against the militants. (Kurdistan 24 via AP)  NO ACCESS KURDISH IRAQHali ilivyokuwa.

Sinjar  (3)

Wanajeshi wa Kikurdi.

This frame grab from Kurdistan 24 video provided to the Associated Press shows smoke believed to be from an airstrike billowing over the northern Iraqi town of Sinjar on Thursday, Nov. 12, 2015. Kurdish Iraqi fighters, backed by the U.S.-led air campaign, launched an assault Thursday aiming to retake the strategic town of Sinjar, which the Islamic State overran last year in an onslaught that caused the flight of tens of thousands of Yazidis and first prompted the U.S. to launch airstrikes against the militants. (Kurdistan 24 via AP)  NO ACCESS KURDISH IRAQMilipuko ikitawala katika Mji wa Sinjar.

Sinjar, Iraq

Wanajeshi wa Kikurdi, Kaskazini mwa nchi ya Iraq wameanzisha oparesheni maalum ya kuukomboa Mji wa Sinjar ulioko karibu na mpaka wa nchi hiyo na Syria kutoka kwa kundi la wapiganaji wa Islamic State (IS).

Oparesheni hiyo inasaidiwa na muungano unaoongozwa na Jeshi la Marekani wakifanya mashambulio ya anga kwa kutumia ndege zao za kivita.

Mji wa Sinjar ulitekwa na kundi la IS mnamo Agosti, 2014. Maelfu ya waumini wa dini ya Yazidi walikwama baada ya kutorokea Mji wa Sinjar. Mamia ya wanaume waliuawa na wanawake wa Yazidi wakatekwa huku wakitumikishwa kwa ngono.

Shambulio hilo la Sinjar lilikuwa moja ya sababu zilizoifanya Marekani kuanza mashambulizi ya angani kusambaratisha ngome za IS nchini Iraq, baada ya hofu kutanda kuwa, huenda kukatekelezwa mauaji ya halaiki nchini humo. Mwezi uliopita Marekani iliongeza mashambulio yake hadi Syria.

Wachambuzi wa mambo wamesema kuwa, kuukomboa Mji wa Sinjar kutaziba mianya ya mawasiliano kati ya ngome mbili za IS Raqqa na Mosul.

Leave A Reply