Walid, Chin Bees, Country Boy walivyowapagawisha mashabiki Usiku wa Kusi (Pichaz + Video)
WAKALI katika Muziki wa Hip Hop Bongo, County Boy, Chin Bees, Walid na Nyandu Tozz wamewapagawisha mashabiki wengi waliofurika katika Usiku wa Kusi Idd Pili ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo MBagala Zakhem jijini Dar.
Katika shoo hiyo iliyoandaliwa na Global Publishers kwa kushirikiana na Wasafi Classic Baby (WCB), kulishuhudiwa mastaa hao wa Hip Hop Bongo wakitumia muda mwingi kuchana na mashabiki mstari kwa mstari huku baadhi yao wakijirusha kucheza na mashabiki.
PICHA: MUSA MATEJA /RICHARD BUKOS -GPL
Comments are closed.