The House of Favourite Newspapers

WANAFUNZI WAFUNDWA FAIDA ZA UPANDAJI WA MITI

Viongozi wa HDIECA, Jielimishe Kwanza na Aspect walipokuwa wakitoa elimu ya mazingira kwa wanafunzi hao.

 

TAASISI isiyo ya kiserikali ya HDIECA inayojishughulisha na mazingira,  leo imewaongoza wanafunzi wa Sekondari ya Mashujaa jijini Dar es Salaam kupanda miti na maua katika maeneo ya shule hiyo.

 

Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Sarah Pima,  amesema lengo la kuwashirikisha wanafunzi hao katika zoezi hilo ni kuwalea vijana katika hali ya kutunza mazingira.

 

Katika tukio hilo, taasisi hiyo ilikuwa na taasisi ya Jielimishe Kwanza na Aspect ambapo iliwafundisha wanafunzi hao mbinu mbalimbali za utunzaji wa mazingira na kujilinda na madhara yanayotokana na mazingira hatarishi kama vile kuvuta hewa isiyofaa na mengineyo.

 

Wanafunzi wakimsikiliza Sarah alipokuwa akiwapa elimu ya mazingira.

 

Wanafunzi wakisikiliza kwa hisia kali

 

Ofisa wa HDIECA, Rabia Bakar, naye aliwapa somo wanafunzi hao (hawapo pichani).

 

Maofisa wa HDIECA wakiwa na wanafunzi.

 

Sarah akiwaongoza wanafunzi kuelekea kwenye zoezi la upandaji miti.

 

Rabia akishirikiana na wanafunzi hao kupanda miti.

 

Sarah akipanda miti na wanafunzi hao

 

…Akiwa na wanafunzi waliokuwa wakijiandaa kupanda maua.

 

JIUNGE NA FAMILIA YA GLOBAL TV UPANDE MTANDAO WA MAFANIKIO

Bofya hapa kujiunga na familia ya Global TV Club ==> Global TV Family Club

Comments are closed.