The House of Favourite Newspapers

WANANCHI WAZIDI KULICHANGAMKIA GAZETI LA SPOTI XTRA

Mkazi wa Mwenge (kushoto) Dar, akisoma gazeti la michezo la Spoti Xtra leo huku akiongozwa na mfanyakazi wa Global Publishers, Keffa.   Hao ni miongoni mwa wasomaji wengi wa gazeti hilo waliolichangamkia katika viunga mbalimbali vya jiji ili kujua habari mbalimbali za burudani na michezo ndani na nje ya nchi.
Dereva wa Bajaj (kulia) akinunua gazeti la Spoti Xtra eneo la Mbezi Tangi Bovu jijini Dar.
Mama muuza matunda ambaye jina lake halikujulikana, akiwa ‘bize’ na gazeti la Spoti Xtra baada ya kulinunua leo asubuhi.
Muuza matunda akiendelea kusoma Spoti Xtra baada ya kulinunua leo eneo la Goba.
Muuzaji wa magazeti ya Spoti Xtra akiuza magazeti hayo ambayo watu walikuwa wakiyachangamkia.
Dereva wa bodaboda akiwa amepozi na gazeti la Spoti Xtra leo huko Mbezi Mwisho.

GAZETI la Spoti Xtra leo liliendelea kukimbiza tena mitaani katika promosheni iliyofanyika viunga mbalimbali vya jiji la Dar ambayo ilianzia  Mwenge, Mbezi Tanki Bovu, Goba Madole, Goba Njia Nne, Mbezi Mwisho, Mbezi Msuguri, Kimara Mwisho na maeneo mengine. Katika promosheni hiyo wasomaji walionekana kugombea gazeti hilo ambapo waliolisoma kwa mara ya kwanza walifurahia mpangilio wake na habari zilizomo.

(HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS | GLOBAL PUBLISHERS)

Aslay na Nandy Waitendea Haki Subalkheri Mpenzi, Escape One

Comments are closed.