TAASISI ya Twaweza ikishirikisha wadau mbalimbali, leo imefanya mdahalo kutathmini hali na mustakabali wa demokrasia nchini ambapo wadau, wanasiasa na watu mbalimbali wameshiriki.
Mdahalo huo umefanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo ambao ulianza majira ya saa tatu asubuhi hadi saa kumi jioni.
Katika mazungumzo hayo, palikuwa na uwasilishaji wa takwimu za kidemokrasia, mjadala huru, maigizo na maonyesho ya sanaa za kidemokrasia.
Mwongozaji wa mdhalo huo alikuwa ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Twaweza ambapo miongoni mwa watu wengine walikuwa ni mmilili wa mtandao wa Jamii Forum, Maxence Melo; Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe; na John Shibuda wa Baraza la Vyama vya Siasa.
NA DENIS MTIMA/GPL