Baadhi ya akina mama wakisikiliza kwa makini mafunzo kutoka kwa wazungumzaji.
Mzungumzaji, Harris Kapiga, akifafanua jambo.
Mzungumzaji, Maza Sinare ‘Maznat’, akifundisha.
Elie akisisitiza moto wa masomo.
Mhariri wa gazeti la Uwazi, Elvan Stambuli (mwenye kofia nyekundu) akiwa katika picha ya pamoja na mzungumzaji Maznat na baadhi ya watu walioshiriki semina hiyo.
WANAWAKE jijini Dar wamejitokeza kwa wingi kwenye semina ya ujasiriamali iliyofanyika Machi 13 mwaka huu katika Ukumbi wa Kamanyola, Sinza, ambapo walipata wasaa wa kujifunza njia mbalimbali za kujikwamua kiuchumi na kujitegemea kupitia kauli mbiu ya ‘Mwanamke ni Familia’.
Semina hiyo iliyodhaminiwa na Global Publishers kupitia shindano lake la Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba, iliratibiwa na shirika la masuala ya maendeleo ya kijamii, Community Development Forum (CDF)na kuhudhuriwa na wazungumzaji mbalimbali wakiwemo: Dk. Elie, Maznat, Harris Kapiga na Mhariri wa gazeti la Uwazi, Elvan Stambuli.
(Picha/Gabriel Ng’osha na Chande Abdallah / GPL)