Wasanii Kuanza Kulipwa Mirahaba
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan leo Juni 15, amesema Serikali imeimarisha usimamizi wa hakimiliki za wasanii na kuanzia mwezi Disemba, 2021 wasanii wataanza kulipwa mirahaba yao kutokana na kazi zinazotumiwa kwenye Runinga, Redio na Mitandaoni.
“Sanaa na utamaduni, sekta hii imekuwa ikikua kwa kasi, miongoni mwa hatua tulizochukua ni kuimarisha usimamizi wa haki miliki za wasanii, nataka kuarifu vijana kuwa kuanzia Disemba mwaka huu wasanii wataanza kulipwa mirabaha yao kutokana na kazi zinazotumiwa kwenye Runinga, Redio na Mitandaoni.” – Rais Samia kwenye mkutano wa vijana Mkoani Mwanza.
Rais Samia amehitimisha ziara ya siku tatu ya kikazi kwa kuhutubia vijana wa Mwanza na kuzindua meli mbili na chelezo moja zilizokarabatiwa katika bandari mkoani humo