Wasanii Waahidi Makubwa Mbele Ya Rais Magufuli
Bodi ya Filamu nchini leo imewaongoza wasanii wa muziki na maigizo na wengineo katika kikao cha mwisho cha maandalizi ya tamasha la kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere litakalofanyika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere uliopo Posta jijini Dar
Katika mkutano huo ambao mgeni rasmi atakuwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli wasanii mbalimbali wameahidi kushiriki na kutoa burudani.
Rais Magufuli anatarajiwa kupewa tuzo na wasanii hao kutokana na umahiri wake wa kazi unaoendana utendaji wa Hayati Baba wa Taifa. Katika kuhitimisha tamasha hilo wasanii hao watakwenda kutoa burudani ya bure kwenye viwanja wa Zakhem vilivyopo Mbagala Dar.
HABARI:NEEMA ADRIAN | PICHA: RICHARD BUKOS
Comments are closed.