The House of Favourite Newspapers

Wasanii Wauaga Mwili wa Mzee Majuto Karimjee (Picha + Video)

Mke wa mzee Majuto aitwaye Aisha Yusuf (katikati) akiwa katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
Staa wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ (katikati) akiwa kabeba jeneza lenye mwili wa marehemu.
Staa wa Bongo Movie,Wema Sepetu akiwa katika viwanja vya Karimjee kuaga mwili wa marehemu Amri Athumani ‘Mzee Majuto’ .
Wasanii wa Bongo Muvi wakijadiliana jambo.
Mke wa Mzee Majuto aitwaye Aisha Yusuf (kulia)
Mwigizaji wa Bongo Movies, Salma Jabu ‘Nisha’ akilia kwa uchungu.

MAMIA ya waombolezaji wamejitokeza katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam kuaga mwili wa aliyekuwa muigizaji nguli wa vichekesho nchini, Amri Athumani ‘Mzee Majuto’ leo Agost 9, 2018.

 

 

Mzee King Majuto alifariki dunia jana Agosti 8, 2018 majira ya saa 2:00 usiku katika Hospitali ya Taifa, Muhimbili alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu kwa siku kadhaa.

 

 

Baada ya kuaga,  mwili ulisafirishwa kwenda nyumbani kwake jijini Tanga kwa maziko ambayo yatafanyika kesho Ijumaa.

 

Baadhi ya wasanii waliofika Wema Sepetu, Salma Jabu ‘Nisha’, Steve nyerere, Diamond Platnumz, Ray, Shamsa Ford, Rich Mavoko, Rommy Jones na wengineo wengi.

 

(PICHA: RICHARD BUKOS | GPL)

DIAMOND Alivyobeba Mwili wa Majuto Leo

WEMA Alivyotinga Msibani Kuagwa Mzee Majuto Karimjee

Comments are closed.