The House of Favourite Newspapers

Wasomaji wa Amani wachangamkia ‘Shinda Nyumba’ Biafra

0

1.Msomaji wa Gazeti la Amani, Crispin Rojas (kushoto) akijaza kuponi yake ili kushiriki bahati nasibu ya Shinda Nyumba. Katikati ni Ofisa Masoko wa Global,Yohana Mkanda. Msomaji wa gazeti la Amani, Crispin Rojas (kushoto) akijaza kuponi  ili kushiriki bahati nasibu ya Shinda Nyumba. Katikati ni Ofisa Masoko wa Global, Yohana Mkanda.

2. Mkanda (kulia) akimsaidia kujaza kuponi msoamaji wa Gazeti la Amani aitwae,  Abdallah Sufian.Mkanda (kulia) akimsaidia kujaza kuponi msomaji wa Amani aitwaye, Abdallah Sufian.

3.Sufiani (kulia) akipewa maelekeza namna ya kujaza kuponi kwenye Gazeti la Amani.Sufiani (kulia) akipewa maelekezo ya kujaza kuponi kwenye gazeti la Amani.

4. Msumi Hamad naye akielekezwa namna ya kujaza kuponi yake na Mkanda.Msumi Hamad akielekezwa namna ya kujaza kuponi yake na Mkanda.

5. Mdau wa Gazeti la Amani aliyejitambulisha kwa jina moja la ,  Imma (kulia) akipata maelekezo ya kujaza kuponi yake na Ofisa masoko wa Global,Yohana Mkanda.Mdau wa gazeti la Amani aliyejitambulisha kwa jina moja la Imma (kulia) akipata maelekezo ya kujaza kuponi yake kutoka kwa Mkanda.

WASOMAJI wa gazeti la Amani wa eneo la Biafra- Kinondoni Dar, leo walichangamka na kulinunua kwa kujaza kuponi kwa wingi kuelekea droo kubwa ya bahati nasibu ya Shinda Nyumba iliyobakiza siku 21 ambapo mshindi atakabidhiwa nyumba  iliyopo eneo la Salasala Kinondoni, Dar.

Bahati nasibu hiyo inaendeshwa na Kampuni ya Global Publishers wachapishaji wa magazeti ya Championi, Uwazi, Risasi, Amani, Ijumaa na Ijumaa Wikienda.

Ofisa Masoko wa Global Publishers, Yohana Mkanda,  alifika eneo hilo na kukuta wasomaji wa Amani wakiwa na gazeti hilo  na kuwapa maelekezo ya namna ya kushiriki bahati nasibu hiyo.

Mkanda alisema: “ Siku zimebaki 21, wakazi wa Biafra changamkieni fursa hiyo na mshindi wa nyumba anaweza kuwa miongoni mwenu, hivyo nunueni magazeti mengi ya Global  na mjaze kuponi ili kujiongezea nafasi ya kushinda.”

NA DENIS MTIMA/GPL

Leave A Reply