The House of Favourite Newspapers

Wasomaji Wachangamkia  Droo ya Pili ya Shinda Nyumba

0

1.Msomaji wa gazeti la Championi (wapili kushoto) akielekezwa na Maofisa Usambazaji wa Global, Jordan Ngowi (kushoto) na (wapili kulia), Yohana Mkanda.Aliyeshikilia magazeti ni muuzaji wa magazeMsomaji wa Gazeti la Championi (wapili kushoto) akielekezwa na Maofisa Usambazaji wa Global, Jordan Ngowi (kushoto) na (wapili kulia), Yohana Mkanda. Aliyeshikilia magazeti ni muuzaji wa magazeti ya Global.

2.Wasomaji wa Magaeti ya Championi na Ijumaa wa eneo la Kimara Suka wakipewa zawadi ya kofia mara baada ya kununua gazeti kabla ya kuweka kuponi zao kwenye ndoo maalum ili kushiriki droo ya piliWasomaji wa Magazeti ya Championi na Ijumaa wa eneo la Kimara Suka wakipatiwa zawadi za kofia mara baada ya kununua magazeti na kukata kuponi.

3.Zoezi la kukata kuponi na kuweka kwenye ndoo maalum ili kushiriki droo ya pili ya Bahati nasibu likifanyika.…. Wakikata kuponi na kuweka kwenye ndoo maalum ili kushiriki droo ya pili ya Bahati nasibu ya Shinda Nyumba.

4.Ofisa usambazaji, Jordani Ngowi (mwenye fulana nyeupe) akimwelekeza msomaji namna ya kujaza kuponi yake ili kushiriki droo ya pili ya Shinda Nyumba.Ofisa usambazaji wa Global, Jordani Ngowi (mwenye fulana nyeupe) akiwaelekeza wasomaji namna ya kujaza kuponi kwenye gazeti.

5.Ofisa Usambazaji wa Global, Yohana Mkanda (kulia) akimvalisha kofia msomaji baada ya kununua gazeti eneo la Kimara Suka.…. Yohana Mkanda (kulia) akimvalisha kofia msomaji wa Kimara Suka baada ya kununua gazeti.

6.Maofisa wa Global, Ngowi na Mkanda wakimwelekeza Msomaji wa Gazeti la Ijumaa namana ya kushiriki bahati Nasibu hiyo eneo la Kimara Mwisho.Maofisa hao, Ngowi na Mkanda wakimwelekeza msomaji wa Gazeti la Ijumaa namna ya kushiriki Bahati nasibu hiyo eneo la Kimara Mwisho.

7.Zawadi za kofia zikitolewa kwa wasomaji.Zawadi za kofia zikitolewa kwa wasomaji.

8.Ngowi (kulia) akimvalisha kofia msomaji baada ya kuweka kuponi yake kwenye ndoo maalum ili kushiriki droo ya pili ya Shinda Nyumba.Ngowi (kulia) akimvalisha kofia msomaji.

91011.Mkanda (kulia ) akimwelekeza msomaji namna ya kujaza kuponi kushiriki droo ya pili ya shinda Nyumba.Mkanda (kulia ) akimwelekeza msomaji namna ya kujaza kuponi.12..13.Wasomaji wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Global (wenye fulana nyeupe).Wasomaji wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Global (wenye fulana nyeupe).

1415..1617.Mwanadada (katikati) akivalishwa kofia baada ya kumaliza zoezi la kuweka kuponi yake kushiriki droo ya pili ya Shinda Nyumba eneo la Mbezi Mwisho.18. Mwanamama akivalishwa kofia baada ya zoezi la kushiriki kuweka kuponi yake kwenye ndoo maalum kushiriki droo ya pili.Wasomaji wakivalishwa kofia baada ya kumaliza zoezi la kuweka kuponi kwenye ndoo maalum eneo la Mbezi Mwisho.

192021.Wapenzi wasomaji wa magazeti ya Global walipoluizunguka gari la matangazo la Global eneo la Mbezi Mwisho ili kuweza kununua gazeti na kushiriki droo ya pili inayotarajiwa kuchezeshwa.Wasomaji wa Mbezi Mwisho wakiwa wamelizunguka gari la matangazo la Global ili wanunue magazeti.

22. Hali ilivyoonekana eneo hilo la Mbezi Mwisho baada ya kufika gari la matangazo.… wa eneo la Mbezi Mwisho wakichangamkia kununu magazeti.

232425.Wasomaji wa magazeti ya Global wakiweka kuponi zao kwenye ndoo maalum kwa ajili ya kushiriki droo ya pili ya Bahati nasibu inayotarajiwa kuchezeshwa mwanzoni mwa mwezi ujao.Wakiweka kuponi zao kwenye ndoo maalum ili kushiriki droo ya pili ya Bahati nasibu itakayochezeshwa mwanzoni mwa mwezi ujao.

WASOMAJI wa magazeti pendwa ya Uwazi, Amani, Ijumaa, Risasi na Ijumaa Wikienda pamoja na yale ya michezo ya Championi wamezidi kujitokeza kwa wingi katika kuchangamkia fursa ya droo ya pili ya Bahati nasibu ya Shinda Nyumba inayoendeshwa na Global Publishers.

Kampuni hiyo leo jijini Dar imetoa zawadi kwa wasomaji wake baada ya kununua magazeti kwa wingi ili kukata kuponi kwa ajili ya kushiriki Bahati nasibu hiyo inayotarajiwa kuchezeshwa mwanzoni mwa mwezi ujao.

Baadhi ya wasomaji waliojinyakulia kofia zilizo na nembo ya Shinda Nyumba ni pamoja na wakazi wa Kimara Suka, Mbezi mwisho na Kinyerezi na kwingineko.

Kupitia Bahati nasibu hiyo msomaji anachotakiwa kufanya ni kununua nakala moja au zaidi ya magazeti na kukata kuponi moja iliyo katika kila gazeti kisha kujaza jina lake kamili na anuani yake na kutuma kwa njia ya Posta, kuipeleka moja kwa moja katika ofisi za Global Publishers zilizoko Bamaga-Mwenge au kuzipeleka kwa mawakala wa kuuza magazeti popote ulipo nchini.

Aidha nyumba inayoshindaniwa imejengwa eneo la Salasala-Kinondoni,  jijini Dar es Salaam, ikiwa na samani za ndani na  itatolewa mwishoni mwa mchezo huku droo nyingine ndogo zikichezeshwa kila mwezi, ambapo simu mpya za kisasa, runinga na ving’amuzi hutolewa.

Katika shindano hili watu walio chini ya umri wa miaka 18, ndugu wa wafanyakazi wa Global Publishers hawaruhusiwi kushiriki.

Na Denis Mtima/Gpl

 

Leave A Reply