The House of Favourite Newspapers

Wastara Juma Ajitosa Bongo Fleva

Staa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma.

STAA wa filamu za Kibongo, Wastara Juma baada ya kusikika kwa Wimbo wa Wanawake ambao aliuzindua wakati akienda nchini Sweden, sasa amejipanga kutoa wimbo mwingine unaoitwa Mama na Mtoto ambao nao unaihusu jamii kwa ujumla.

 

Akibonga na Risasi Vibes, Wastara alisema kuwa ameamua kuimba nyimbo zinazoihusu jamii hasa akina mama na watoto.

 

“Wimbo wangu wa sasa unaelezea zaidi thamani ya mtoto na akina mama jinsi ya kumlinda mtoto, nimeshatoa ‘single’ yake na video ndiyo namalizia kuifanyia shooting hivyo watu wakae mkao wa kula,” alisema Wastara.

Comments are closed.