Watani wa Jadi Kukutana Juni 25 – TPLB Yatoa Tamko Rasmi
RASMI Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara, (TPLB) imeusogeza mbele mchezo wa Kariakoo Dabi ambao ni namba 184 kati ya Yanga SC vs Simba SC uliopangwa kuchezwa Juni 15 2025, Uwanja wa Mkapa.
Taarifa rasmi iliyotolewa Juni 13 2025 na TPLB imeeleza imeusogeza mbele mchezo huo wa watani wa jadi mpaka Juni 25 2025.
Taarifa hiyo imeeleza namba hii: “Bodi ya Ligi Kuu Tanzania, (TPLB) imeusogeza mbele mchezo wa NBC namba 184 kati ya Yanga SC uliotarajiwa kuchezw Juni 15 2025 mpaka Juni 25 2025, bodi inawatakia maandalizi mema.”