The House of Favourite Newspapers

Watu 16 wauawa kwa ajali ya treni Pakistani

0

treniTreni hiyo baada ya kupata ajali.

WATU wapatao 16 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa kwenye ajali ya treni iliyotokea katika Wilaya ya Bolan, jimbo la Baluchistan, Kusini Magharibi mwa Pakistani, jana.

Mamlaka ya Reli nchini Pakistani imethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa, ajali iliyotokea karibu na Mji wa Quetta, Makao Makuu ya jimbo la Baluchistan baada ya breki zake kushindwa kufanya kazi wakati wa ikipandisha mlima hivyo kupelekea kuanguka.

Treni hiyo iliyokuwa na abiria takribani 300, baada ya ajali majeruhi walipelekwa hospitali kwa ndege maalum ya uokoaji iliyowahi kufika eneo la tukio.

Waliokufakwenye ajali hiyo ni abiria 12, dereva wa treni hiyo na msaidizi wake na Maofisa Polisi wawili wa Mamlaka ya Reli.

Ajali nyingine kama hiyo ilitokea nchini Pakstani Julai 17, mwaka huu iliyouwa watu baada ya treni maalum ya mafunzo ya kijeshi ilipoanguka baada ya kuvunjika kwa daraja.

Leave A Reply