The House of Favourite Newspapers

Wauzaji Wa Magazeti Wang’ara Global

Baadhi ya wauza magazeti wa kongwe wa Kampuni ya Global Publishers LTD,wakiwa katika pozi la pamoja baada ya kutunukiwa vyeti vya uuzaji bora wa magazeti ya Championi,Spoti Xtra, Ijumaa,Ijumaa Wikienda,Risasi, Amani na Uwazi.

 

ILIKUWA ni shangwe ndani ya Ofisi za Global Publishers zilizopo Sinza-Mori jijini Dar jana baada ya wauzaji wa magazeti 16 kupewa vyeti kutokana na mchango wao wa kuwa na kampuni kwa zaidi ya miaka 10.

 

Wauzaji hao waliokabidhiwa zawadi zao ni wale wanaotokea jiji la Dar ambao wametoa mchango wao kwa kampuni kwa muda wote huo hadi sasa.

Mhasibu Mkuu wa Global Publishers LTD, Lawrence Kabende (kulia), akionyesha namna vilivyotengenezwa vyeti hivyo, kabla ya shughuli ya kuwakabidhi wauza magazeti hao kuanza.

Akizungumza katika mkutano huo, muuza magazeti Mohamed Juma Mbunge alisema kuwa, imekuwa jambo kubwa kwani hakuna kampuni iliyowahi kutoa zawadi kama hiyo.

Meneja Mkuu wa Global Publishers LTD, Abdallah Mrisho (kushoto) akimkabidhi mmoja wa wauza magezeti hayo cheti hicho.

“Nitoe shukrani zangu kubwa kwa Eric Shigongo (Mkurugenzi Mtendaji wa Global Group) kwa heshima aliyotupa, tangu nimekuwa muuza magazeti sijawahi kuona kampuni ikifanya kitu kikubwa kama hiki, tunashukuru sana,” alisema Mbunge.

Muuzaji mwingine, Juma Ikhala alipongeza kampuni ya Global kuja na gazeti namba moja la michezo la Spoti Xtra linalotoka kila Jumapili kupunguzwa bei kutoka shilingi 800 hadi 500 na pia kuliongezea siku na kuwepo siku ya Alhamisi.

 

“Nashauri hili Spoti Xtra litoke hata Jumanne tena litakuwa vizuri kwani limeshiba na linastahili, nawapongeza Global kwa hii zawadi,” alisema Ikhala.

 

Comments are closed.