The House of Favourite Newspapers

Wawa Avujisha Siri ya Gomes Simba

0

PASCAL Wawa, beki kisiki wa kikosi cha Simba, amesema kuwa siri kubwa ambayo wanayo katika mapambano ya kuzuia hatari za wapinzani wao ni maneno ya Kocha Mkuu, Didier Gomes, kuwataka wasikubali kufungwa.

 

Katika Ligi Kuu Bara, safu ya ulinzi ya Simba inashika namba moja kwa kuruhusu mabao machache ikiwa ni mabao 9 kabla ya mchezo wa jana dhidi ya Dodoma Jiji, Uwanja wa Mkapa.

 

Safu ya ulinzi ya Mwadui inashika namba moja kwa kufungwa mabao mengi ambayo ni 52 baada ya kucheza mechi 27.

 

Akizungumza na Championi Jumatano, Wawa alisema kuwa kila mara wamekuwa wakisisitizwa na Gomes wasikubali kuokota mpira kwenye nyavu zao hivyo wao wanafuata maelekezo na kutimiza majukumu yao.

“Safu yetu ya ulinzi ina wachezaji wenye kujiamini na wanatimiza majukumu kwa umakini.

 

Ukianza na mimi, pia Onyango (Joash), Kenedy (Juma), hata Nyoni (Erasto). Maagizo ambayo tumepewa na mwalimu (Gomes) tusikubali kufungwa.“Imekuwa hivyo kwenye mechi zetu zote zile za Ligi ya Mabingwa Afrika hata Kombe la Shirikisho tumekuwa tukifanya kazi yetu, hivyo furaha yetu ni kuona kwamba hatufungwi,” alisema Wawa.

Stori: Lunyamadzo Mlyuka, Dar es Salaam

Leave A Reply