POLISI mkoani Shinyanga inawashikilia vijana wawili, Boazi Shija (14)na Jakaya John (14), kwa tuhuma za kumbaka mtoto mwenye miaka sita (jina limehifadhiwa).Watuhumiwa hao ni wakazi wa Kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.
Kamanda wa Polisi Mkoani Shinyanga, ACP Debora Magiligimba, amesema vijana hao walimlaghai mtoto huyo kwa pipi na kumpa hela kisha kumpeleka kichakani karibu na eneo analoishi na wazazi wake kisha kumfanyia unyama huo.
Polisi imesema watawafikisha mahakamani watuhumiwa hao baada ya upelelezi kukamilika.