Wazari Nape Azindua Mnara wa Mawasiliano Kalambo Mkoani Rukwa
UZINDUZI: Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mh. Nape Nnauye @napennauye amezindua mnara wa mawasiliano katika eneo la Kalambo, mkoani Rukwa, uliojengwa kwa ushirikiano kati ya TigoZantel na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF).
Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Tigo akiwemo Meneja wa Tigo Kanda ya kusini Bw. Moses Busee pamoja na Meneja wa Tigo Mkoa wa Rukwa Bw. Fransis Mwasamwene.
Jumla ya minara mipya 46 Tanzania nzima imewekwa ikiwa lengo ni kuendelea kujumuisha wananchi wengi zaidi kwenye huduma za kifedha na za kidigitali.
Hii ni sehemu ya mkakati wa TigoZantel kuwekeza kwenye miundombinu ya mawasiliano.