VIONGOZI mbalimbali wamejumuika na familia ya Eric Shigongo katika ibada ya mazishi ya mama yake, Bi. Asteria Kahabi Kapela, ambaye atazikwa leo Agosti 1, 2018 nyumbani kwake katika kijiji cha Bupandwamhela kilichopo Buchosa, wilayani Sengerema.
Baadhi yao ni Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba ambaye pia ni Mbunge wa Buchosa kupitia CCM, mbunge wa zamani wa Nyamagana na aliyekuwa waziri wa zamani wa mambo ya ndani, Lawrence Marsha.
Mbali namawaziri hao, wengine ni Mchungaji Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ na wengine.
Bi. Asteria Kapela alifariki dunia Ijumaa ya Julai 27, 2018 katika Taasisi ya Jakaya Kikwete Muhimbili jijini Dar es Salaam ambako alikuwa amelazwa akipatiwa matibabu.
Comments are closed.