The House of Favourite Newspapers

Waziri wa Nishati Ahukumiwa Jela Miaka Minne kwa Rushwa

WAZIRI wa zamani wa Nishati wa Zimbabwe, Samuel Undenge,  amehukumiwa kifungo cha miaka minne jela baada ya kupatikana na hatia katika makosa ya rushwa

Waziri huyo aliyefanya kazi kipindi ya Rais Robert Mugabe amekuwa kiongozi wa kwanza kuhukumiwa tangu kiongozi huyo aondolewe madarakani ambapo alituhumiwa kusaini mikataba na kuzilipa kampuni ambazo hazikuwahi kufanya kazi (kampuni hewa) ikiwemo Zimbabwe Power Company (ZPC) kiasi cha dola za Marekani 12,650, (sawa na Tsh. Milioni 28.6) mwaka 2016.

Aidha, wakili wa Undenge amesema atakata rufaa juu ya hukumu hiyo kwa kuwa imekuwa ya kushtua mno

Wakati huohuo, waziri wa zamani wa mambo ya nje, Walter Mzembi,  anakabiliwa na mashitaka ya kutumia vibaya ofisi ya umma ambapo pia waziri wa zamaani wa fedha, Ignatius Chombo,  akishitakiwa kwa makosa ya rushwa. Mawaziri wote hao wamekana mashitaka yao.

Comments are closed.