The House of Favourite Newspapers

We baba fanueliii!!!-15

0

ILIPOISHIA

Alichokifanya ni kumsogelea, alipomfikia tu, kwanza akambipu kwa kuupeleka mkono kiunoni mwa mwanamke huyo, mkono huo ukapokelewa kwa tabasamu pana. Akaona yes, mambo yamejipa. Naye akarudisha kwa tabasamu pana.

ENDELEA NAYO

Mmh!” Mzee Paulo alijikuta akiguna.

“Vipi tena babu?”

“We mwanamke kama kigori, mwili umekaa poa sana, sijawahi kumuona mwanamke kama wewe kwa uzee huu,” alijibu mzee Paulo.

“Kwani wewe ni bingwa wa kutembea na wanawake wengi?”

“Hapana! Simaanishi hivyo! Namaanisha kwamba umeumbika, Mungu alitulia sana siku alipokuumba,” alisema mzee Paulo kwa mbwembwe huku akiiandaa mikono yake kumpokea mwanamke huyo.

Muda huo ulikuwa ni wa mechi tu, hakukuwa na kupiga sana stori kwani kama kupiga hizo stori walipiga sana kwenye simu. Mzee Paulo akaiandaa mikono yake, akampokea mwanamke huyo na kwa hara, kilichofuata kitandani hapo ni milio ya kitanda kikilalamika kwamba kinaumizwa huku kwenye kila hatua miguno ya mahaba ilizidi kuongezeka.

“Ashiii…ooooh! Hapohapo…” alisema mama Zubeda huku akilalamika tu, kadiri kitanda kilivyokuwa kikizidi kupiga kelele, naye akazidi kuweweseka.

“Cheza kama upo ngomani, katika kama upo kwenye mashindano ya khanga moko,” alisema mzee Paulo huku akimshikashika mama Zubeda maungoni.

***

Wakati kazi yake ikifanywa na mzee Paulo, huku nyumbani baba Fanueli hakutaka kutulia, kila wakati alikuwa akiangalia simu yake, kichwa chake kilichanganyikiwa, kwa mara ya kwanza katika mwaka huo akajikuta akimuomba Mungu amfanikishie kile alichokuwa akikitaka, picha zipigwe mwanamke huyo akiwa chumbani.

“Vipi mume wangu?’ aliuliza mama Fanueli.

“Vipi nini?”

“Unaonekana una mawazo, tatizo nini?”

“Hakuna kitu.”

“Halafu mbona siku hizi hata haki yangu hutaki kunipa?”

“Sijisikii vizuri, naumwa viungo sana.”

“Mmmh!”

“Ndiyo hivyo.”

Kulikuwa na idadi kubwa ya wanawake kichwani mwake, hapo alikuwa akijifikiria ni kwa nani alitakiwa kwenda wakati huo. Kwa akina Tunda, Mariamu na wanawake wengine alikwenda sana na kila alipofikiria ni mwanamke gani alitakiwa kumfuata kwa wakati huo, hakupata jibu.

“Ila Rose si yupo! Ngoja nimtafute, kitambo kweli sijamuona,” alisema baba Fanueli, hapohapo akachukua simu yake na kuanza kulitafuta jina la Rose.

“Upo wapi mrembo?” aliuliza mara baada ya simu kupokelewa.

“Eeh!”

“Unashangaa nini?”

“Kunipigia! Tangu lini?”

“Jamani! Kwani kuna kosa nikimpigia malkia wangu?”

“Hakuna kosa, ila ulinitenga sana, ukanisusa mno,” alisema Rose.

“Hakuna kitu kama hicho! Nilikuwa bizebize kidogo, si unajua tunakuwa na kazi nyingi. Hebu niambie, upo nyumbani?” alisema baba Fanueli na kuuliza.

“Nipo nimejaa tele! Unataka kuja?”

“Pigia mstari. Nakuja.”

Hakutaka kukaa nyumbani, hakutaka kusikia lolote lile, alichokitaka ni kuondoka kuelekea nyumbani kwa Rose ambapo hakukuwa mbali na hapo alipokuwa akiishi. Akaingia chumbani, akajiandaa tayari kwa kuondoka.

“Unakwenda wapi?”

“Kutembea, nakwenda baa kupoteza mawazo.”

“Wewe si umesema viungo vinauma?”

“Ndiyo! Kwani baa nakwenda kufanya mazoezi? Si nakwenda kukaa tu.”

“Basi twende tukakae wote.”

“Weee…hakuna kitu kama hicho. Unataka walevi wakanikonyezee mke wangu? Baki na nyumba,” alisema baba Fanueli huku akionekana kumaanisha alichokisema, kwa sababu yeye alikuwa mtu wa wanawake, kwa mkewe alisikia wivu mno.

“Hakuna mtu wa kunikonyeza wala kunitongoza, lazima leo twende wote huko baa,” mama Fanueli alimwambia.

“Hivi wewe mwanamke mbona huelewi ukiambiwa jambo, nimesema hivi, siendi na wewe, wewe baki na nyumba,” baba Fanueli alimwambia mkewe.

***

Mzee Paulo hakutaka kuchelewa, akamwambia mama Zubeda ampe mgongo kwani kuna ufundi mkubwa alitaka kumfanyia, mwanamke huyo akafanya hivyo. Mzee huyo hakutaka kuchelewa, hapohapo akatoa simu yake na kuanza kumpiga picha za mgongoni mwanamke huyo, tena kisiri.

Mama Zubeda hakugundua kitu, simu haikutoa sauti, alipomaliza, akaificha na kumwambia amkalie kwa juu, tena huku akifumba macho kimahaba, mwanamke huyo pasipo kujua chochote, akafanya kila alichoambiwa, kilichofuata ni kupigwa picha tu huku akiwa ameyafumba macho yake kimahaba.

“Kwisha habari yake,” alisema mzee Paulo, akakenua meno yake yote thelathini na mbili, akaona kazi yake imekwisha.

Leave A Reply