The House of Favourite Newspapers

WEMA ASHAURIWA KUONGEZA ‘TUNYAMA’

WANANZENGO hawaishiwi maneno. Baada ya mwanadada Wema Sepetu kuamua kujipunguza mwili, basi unaambiwa eti wanamshauri aongeze nyama kidogo (tunyama) maana amepungua sana.Kauli hiyo ya wananzengo imekuja kufuatia Wema kutupia picha zake mpya akiwa na Petit Man ndipo walipoibuka na kuanza kumshauri.

“Huu mwili hapana jamani mbona haumnogei kabisa da Wema? Hivi hakuna namna anaweza kuongeza ongeza tunyama labda,” aliandika malkia wa udaku. Wema ambaye alikuwa chibonge zamani, kwa sasa amepungua na inaelezwa kuwa ndivyo mwenyewe alivyoamua kuwa.

Comments are closed.