The House of Favourite Newspapers

Wema, JB wamuigiza Diamond

0

wema3 Wema Isaac Sepetu.

Deogratius Mongela na Mayasa Mariwata 

Wamerudi! Mastaa wawili wa Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu na Jacob Steven ‘JB’ wameachia filamu mpya ambayo ndani yake wanadaiwa kumuigiza mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ inayokwenda kwa jina la Chungu cha Tatu ambapo ndani yake, kila mwanaume anayekuwa na Wema anashindwa kudumu naye kwa sababu anampenda mwanamuziki huyo.

jbJacob Steven ‘JB.

Habari zilizolifikia Ijumaa Wikienda zilieleza kuwa filamu hiyo inalenga uhusiano uliokuwepo kati ya Wema na Diamond ambapo mwanadada huyo amekuwa akiachana na mwanamuziki huyo na kurudiana naye licha ya kutembea na mashosti zake.

Leave A Reply