The House of Favourite Newspapers

WEMA SEPETU: SIWEZI KURUDIANA NA X- WANGU JAMANI!

0

MUIGIZAJI mwenye nyota ya kipekee Bongo, Wema Sepetu ‘Keki ya Taifa’, amekanusha ishu ya inayovuma mitandaoni kuwa anatamani kurudiana na X-wake ambaye ni Mbongo Fleva, kwa kusema hawezi kamwe kurudiana naye kwani mpenzi wake wa sasa anampa furaha ya kutosha.

Wema alifikia hatua ya kuandika ujumbe wa kukanusha skendo hiyo, baada ya hivi karibuni kuenea kwa ubuyu kuwa yeye na Mbongo Fleva huyo wamerudiana tena, anadiriki hadi kwenda kwake kupika, jambo ambalo lilimchanganya na kuamua kulitolea ufafanuzi.

Wema na X-wake huyo, waliwahi kuwa ‘Couple’ ambayo ilitikisa jiji, baadaye wakamwagana na kisha X-wake huyo kujiingiza kwenye ulimwengu wa huba na mfanyabiashara maarufu, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss lady’ ambapo amezaa naye watoto wawili, lakini pia ni baba wa mtoto wa mwanamitindo Hamisa Mobeto anayeitwa Prince Abdul.

NA ISRI MOHAMED/GPL

 

Leave A Reply