The House of Favourite Newspapers

Wentworth Gas Ltd Yasaidia Wasichana wa Shule Za Kitanzania Kwenye Sekta ya Elimu

0
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Ahmed Abbas Ahmed (katikati) akipokea taulo za kike kwa ajili ya wanafunzi wa shule tisa za msingi mkoani Mtwara kutoka kwa Meneja wa huduma za Uwajibikaji kwa jamii wa Kampuni ya Wentworth Gas Ltd, Bi Neema Ndikumwami (wapili kulia) katika hafla ya kusherehekea siku ya kumbukizi ya kuzaliwa Rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania DKT. Samia Suluhu Hassan iliyofanyika katika uwanja wa Mashujaa, Mjini Mtwara. (Kulia) ni Mkuu wa shule ya Msingi ya Kambarage Mtwara, Bi. Florence Magomba na (kulia wa tatu) ni Mkurugenzi wa FB Empowerment Bi. Fidea Bright. (Kushoto) ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mtwara Mhe. Shadida Ndile.

27 Januari 2023, Mtwara. Kampuni ya Wentworth Gas Ltd, kupitia Taasisi ya Wentworth Africa Foundation Tanzania imetoa taulo 1,500 zenye thamani ya Shilingi milioni 5 kwa watoto wa shule za Mtwara ikiwa ni sehemu ya mpango wake wa uwajibikaji kwa jamii.

Akizungumza katika hafla hiyo mjini Mtwara, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali. Ahmed Abbas Ahmed aliishukuru kampuni ya Wentworth Gas Ltd kwa msaada wao katika kuhakikisha wasichana wanabaki shuleni.

Meneja wa huduma za Uwajibikaji kwa jamii wa Kampuni ya Wentworth Gas Ltd, Bi Neema Ndikumwani (wapili kulia) akimkabidhi mwanafunzi wa shule ya Kambarage taulo za kike katika hafla ya kusherehekea siku ya kumbukizi ya kuzaliwa Rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania DKT. Samia Suluhu Hassan iliyofanyika katika uwanja wa Mashujaa, Mjini Mtwara.

Meneja Mkazi wa Kampuni ya Wentworth Gas Ltd, Richard Tainton alisema kuwa kama sehemu ya mpango wa uwajibikaji kwa jamii wa Wentworth, wana programu mbalimbali za kusaidia sekta za Afya, Elimu na Mazingira katika eneo hilo.

Wanafunzi Pamoja na wakuu wa shule kutoka shule 6 za msingi mjini Mtwara pamoja na uogozi wa mkoa wa Mtwara wakiwa kwenye hafla ya kusherehekea siku ya kumbukizi ya kuzaliwa Rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania DKT. Samia Suluhu Hassan iliyofanyika katika uwanja wa Mashujaa, Mjini Mtwara.

‘Nina furaha kuthibitisha kuwa kampuni ya Wentworth Gas kupitia Asasi ya Wentworth Africa Tanzania inaendelea kusaidia jamii ambazo tunafanyakazi kama sehemu ya mpango wetu wa kurudisha kwa jamii. Programu yetu inayoitwa “Keep a Girl in School” unawapa wasichana fursa ya kupata huduma salama na zinazofaa, kama vile vyoo, majisafi, mifumo ya kudhibiti taka na vifaa vya  usafi wa hedhi.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Ahmed Abbas Ahmed (wapili kutoka kushoto) pamoja na Katibu Tawala wa Mkoa, Abdallah Malela (kushoto), Mkurugenzi wa FB Empowerment Bi. Fidea Bright (wapili kutoka kulia) na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mtwara Mhe. Shadida Ndile (kulia) pamoja na wafanyakazi kutoka Kampuni ya Wentworth Gas Ltd katika hafla ya kusherehekea siku ya kumbukizi ya kuzaliwa Rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania DKT. Samia Suluhu Hassan iliyofanyika katika uwanja wa Mashujaa, Mjini Mtwara.

Wasichana ambao wanaweza kusimamia usafi wao wa hedhi na kubaki shuleni wana uwezekano mkubwa wa kumaliza elimu yao, ambayo inaweza kuwa na manufaa ya muda mrefu ya kiuchumi. Tunaendelea kushirikisha serikali katika ngazi zote ikiwa ni pamoja na jamii zenyewe ili kutambua na kuleta athari popote tunapoweza ili kuboresha maisha ya watu ‘- Meneja Mkazi Wentworth Gas Ltd, Richard Tainton.

Kuhusu Wentworth Resources PLC:

Wentworth ni kampuni inayojitegemea iliyoorodheshwa na AIM na mshirika katika Washirika wa pamoja wa Mnazi Bay (pamoja na TPDC, M&P, na CMBL). Kampuni hii inaongoza kwa uzalishaji wa gesi nchini Tanzania. Lengo letu kuu la uzalishaji huko Mnazi Bay, katika mwambao wa bonde la mto Ruvuma, Kusini mwa Tanzania. Kwa historia yetu nzuri na utendaji mzuri wa kifedha, tunafanya kazi kwa karibu na washirika wetu kusaidia Tanzania katika kufikia upatikanaji wa nishati kwa wananchi wote ifikapo 2030.

Kwa habari zaidi, tafadhali wasiliana na:

Neema Ndikumwami

Meneja wa Uwajibikaji kwa Jamii

+255 (0) 786 716 318

[email protected]@wentplc.co.tz

Leave A Reply