The House of Favourite Newspapers

Weusi ndiyo basi tena

1

weusiKUNDI maarufu zaidi kwa sasa la hip hop nchini, Weusi limeweka wazi kumaliza kufyatua kazi zake kwa mwaka huu baada ya kutoa ‘hit songs’ kadhaa wiki chache zilizopita na kuwataka mashabiki wake kuwasubiri upya mwakani.

Hivi karibuni, kundi hilo kupitia memba wake, Nikki wa Pili, alitoa Baba Swalehe na Joh Makini akaachia Don’t Bother aliomshirikisha AKA wa Afrika Kusini, huku Original ya G Nako ikitarajiwa kuwa hewani muda wowote kuanzia sasa.

Hata hivyo, Nikki ameliambia Championi Jumatano, kuwa kazi moja iliyobaki ni ya Bonta pekee ambayo nayo ipo jikoni na itatoka kabla ya mwaka huu kumalizika, hivyo kufunga hesabu za kazi za Kampuni ya Weusi kwa mwaka huu. Wimbo huo wa Bonta unaitwa Usirudi Jela aliomshirikisha Belle 9 na Nikki.

“Tunashukuru tumetambulisha kazi mbili hivi karibuni na zimeeleweka, itatoka Original ya G Nako kisha itafuata ya Bonta ambayo ipo jikoni na baada ya hapo itakuwa mwisho kwa mwaka huu mpaka mwakani, tunashukuru mashabiki wetu kwa kuwa nasi na tunaamini tutaanza pamoja mwakani,” alisema Nikki.

1 Comment
  1. noriega ulomi a.k.a hb melki king says

    mbona hadithi na mikasa hazifunguki?

Leave A Reply