Mratibu mkuu wa shindano hilo Bw,Solomon akizungumza jambo na waandishi wa habari.
Meneja wa Diamond Babu Tale naye akiwaelezea waandishi (hawapo pichani) akiwaambia jinsi msanii wake atakavyolishika jukwaa siku hiyo.
Muakilishi wa kinywaji cha New Crove (kushoto) ambaye ni mmoja wa wawadhamini akizungumza pia
Wasemaji na waandaji wa tamasha hilo wakiwa katika picha ya pamoja.
Na Imelda Mtema
Mwanamuziki mahiri kutoka Nigeria, Wizkid anayetarajia kutumbuiza jijini Dar es Salaam Oktoba 31 mwaka huu atasindikizwa na wanamuziki mahiri wa hapa Bongo ambao ni Nassib Abdul ‘Diamond’ ,Christian Bella na Farid Kubanda ‘FID Q’
Akisungumza kwenye mkutano wa waandishi wa habari katika ukumbi wa Solomon,uliopo Namanga jijini Dar mratibu mkuu wa Shoo hiyo Bw,Solomon alisema kuwa wamewachagua wanamuziki hao kupanda jukwaa moja na mwanamuziki huyo kwa kuwa wao ni wakali pia.
Kumbuka viingilio vya onesho hili kubwa la burudani siku ya jumamosi ni shilingi elfu 20,000 kwa viti vya kawaida na viti maalum ni shilingi laki 100,000