The House of Favourite Newspapers

Wolper akimbilia Arusha

PAMOJA na Jiji la Dar kuwa na fursa nyingi na burudani kama zote, lakini kwa staa wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper, mambo ni tofauti kwani ameamua kutoka nduki na kuhamishia makazi yake jijini Arusha.

Wolper ameliambia Gazeti la Ijumaa kuwa, ameamua kuhamishia makazi yake Arusha kwa kwa sababu maisha ya Dar yamemchosha hivyo ameona abadilishe hali ya hewa.

“Kwa sasa nipo Chuga (Arusha), nimeamua kubadilisha hali ya hewa, lakini biashara zangu zinaendelea kama kawa kule Tandika (Dar), siyo lazima wote tusongamane Dar,” alisema Wolper akikanusha tetesi kuwa amefulia.

Stori: Imelda Mtema, Dar

Comments are closed.