The House of Favourite Newspapers

Yacouba Amerudi Huko Yanga, Kazi Mnayo

0

DAKTARI wa Yanga Nahumu Muganda amewaondoa hofu mashabiki wa timu hiyo kwa kuwaambia kiungo wao mshambuliaji Mburkinabe Yacouba Songne yupo fiti kwa ajili ya michezo ijayo ya Ligi Kuu Bara na Kombe la FA.

 

Yacouba yupo nje ya uwanja tangu kwenye mchezo wa hatua wa Robo Fainali ya Kombe la Mapinduzi akisumbuliwa na maumivu ya misuli huko akikosa michezo kadhaa ya ligi.

 

Mshambuliaji huyo kabla ya kupata maumivu hayo alikuwa sehemu ya kikosi cha kwanza cha Mrundi Cedric Kaze ambaye kwenye michezo ijayo ataanza kuonekana uwanjani.

 

Akizungumza na Championi Jumatano, Muganda alisema kuwa mshambuliaji huyo alianza mazoezi magumu ya pamoja na timu hiyo juzi Jumatatu, baada ya kuingia kambini huko Kimbiji, Kigamboni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Muganda alisema kuwa kwa Yacouba yupo fiti kucheza mchezo ujao kama kocha akihitaji kumtumia katika michezo ijayo ya ligi ukiwemo unaofuatia dhidi ya Coastal Union.Aliongeza kuwa tofauti na kiungo huyo kupona wengine ni beki Abdallah Shaibu ‘Ninja’ na kipa namba tatu Ramadhani Kabwili waliokuwa na majeraha tofauti.

 

“Yacouba amepona na sasa yupo fiti kuanza kuichezea Yanga katika michezo ijayo ya ligi na mashindano mingine tunayoshiriki katika msimu huu.

 

“Jana (juzi) Jumatatu alianza mazoezi ya pamoja na timu, mara baada ya timu kurejea kambini baada ya mapumziko ya siku moja waliyopewa wachezaji.

 

“Tulikuwa na majeruhi saba pamoja na Mukoko (Tonombe) ambaye yeye aliumia mechi dhidi ya Mtibwa Sugar, Kabwili na Ninja ambao wenyewe wamepona wamerejea uwanjani, hivyo wamebakia watatu pekee ambao ni Said Ntibazonkiza, Dickson Job na Balama Mapinduzi,” alisema Muganda.

Leave A Reply